10 May 2024 / 112 views
Tetesi za soka Ulaya

Manchester United hawana nia ya kumfukuza meneja Erik ten Hag kabla ya fainali ya Kombe la FA mnamo Mei 25.

Kocha wa Bayern Munich Thomas Tuchel ana nia ya kuwa meneja wa Manchester United iwapo klabu hiyo itaamua kumfukuza Ten Hag.

Tuchel ndiye mgombea anayeongoza kuchukua mikoba Old Trafford, lakini kocha wa Sporting Lisbon Ruben Amorim na meneja wa zamani wa Chelsea Graham Potter pia wako kwenye kinyang'anyiro.

Meneja wa zamani wa Manchester United Jose Mourinho angependa kurejea kwa kipindi cha pili lakini klabu hiyo haitaki kumteua tena Mreno huyo mwenye umri wa miaka 61, ambaye alitimuliwa na Roma mwezi Januari.

Crystal Palace wako tayari kumuuza mlinzi wa Uingereza Marc Guehi, 23, badala ya kumtoa winga wa Ufaransa Michael Olise, 22, au winga wa Uingereza Eberechi Eze, 25, msimu huu.

West Ham wameanza mazungumzo ya kumsajili winga wa Corinthians, 19, raia wa Brazil, Wesley Gassova, ambaye pia analengwa na Liverpool.

Chelsea inatafuta mnunuzi wa mshambuliaji wa Albania Armando Broja kufuatia kipindi cha mkopo cha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 na Fulham.

Chelsea wako kwenye mazungumzo ya kumsajili winga Estevao Willian mwenye umri wa miaka 17 kutoka Palmeiras.

The Blues pia wamemtambua mlinda lango wa Everton Muingereza Jordan Pickford, 30, kama wanayemlenga majira ya joto.