06 May 2022 / 180 views
Acelotti awamwagia sifa wachezaji wake

Kocha wa Real Madrid, Carlo Ancelotti amesema kuwa "historia ya klabu" ilisaidia timu yake ya Real Madrid kutinga fainali ya UEFA.

Mabingwa hao mara 13 wa Uropa walitoka nyuma kwa 1-0 usiku na kwa jumla ya 5-3 katika hatua ya nne ya mwisho kuingia dakika ya 90, lakini Rodrygo alifunga mabao mawili ya dakika za mwisho na mkwaju wa penalti wa Karim Benzema wa dakika za nyongeza ukawafanya wapite.

Real pia walikuwa wametoka nyuma na kuwashinda Paris Saint-Germain katika hatua ya 16 bora na Chelsea katika robo fainali.

"Siwezi kusema tumezoea kuishi maisha ya aina hii, lakini kilichotokea usiku wa leo kilitokea dhidi ya Chelsea na pia dhidi ya PSG," Ancelotti aliiambia BT Sport baada ya kuwa kocha wa kwanza katika historia kutinga fainali tano kwenye mashindano hayo.

“Ikibidi useme kwa nini, ni historia ya klabu hii ndiyo inatusaidia kuendelea pale inapoonekana tumeondoka.

"Mchezo ulikuwa karibu kumalizika na tulifanikiwa kupata nguvu ya mwisho tuliyokuwa nayo."

Ushindi huo wa jumla ya 6-5 unaipeleka Madrid kwenye fainali ya 17 ya Ligi ya Mabingwa iliyoongeza rekodi, ambapo Ancelotti anaweza kuweka rekodi mpya ya Vikombe vinne vya Uropa akiwa kocha.

Washindi mara sita Liverpool watakuwa wapinzani wao katika fainali itakayofanyika tarehe 28 Mei mjini Paris.

"Nina furaha kuwa pale kwenye fainali, mjini Paris dhidi ya mpinzani mwingine mkubwa," aliongeza Ancelotti mwenye umri wa miaka 62.

Ancelotti pia amekuwa kocha wa kwanza kushinda ligi zote tano bora za Ulaya wakati Real iliponyakua ubingwa wa LaLiga wikendi iliyopita.