13 Jan 2021 / 260 views
Tottenham kucheza na Fulham leo

Tottenham watacheza na Fulham Jumatano katika mabadiliko ya mechi baada ya mechi ya Ligi Kuu ya Tottenham dhidi ya Aston Villa kuahirishwa kwa sababu ya visa vya coronavirus kwenye kambi ya Villa.

Mechi ya nyumbani ya Fulham dhidi ya Chelsea iliyotakiwa kufanyika Ijumaa sasa itafanyika siku ya Jumamosi.

Aston Villa, ambao walitarajiwa kuikaribisha Everton Jumamosi, watawakaribisha The Toffees siku ya Jumapili chini ya orodha iliyofanyiwa marekebisho.

Mchezo wa Fulham huko Tottenham hapo awali ulipangwa kufanyika 30 Desemba. Lakini uliahirishwa kwa sababu ya mlipuko wa coronavirus huko Fulham.

Ligi za chini huko Scotland zimesimamishwa Mchezo wa Celtic licha ya wachezaji 13 kutokana na maambukizi ya ugonjwa wa Corona.

Jumatano - Tottenham dhidi ya Fulham 20:15 (Awali Desemba 30)

Jumamosi - Fulham dhidi ya Chelsea 17:30 (Awali Ijumaa)

Jumapili - Aston Villa v Everton 12:00 (Awali Jumamosi)