30 Jun 2020 / 130 views
Solskjaer awapa somo washambuliaji wake

Kocha wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer amesema kumekuwa na maboresho katika safu yake watatu Anthony Martial, Marcus Rashford na Mason Greenwood msimu huu.

Rashford na Martial wamechangia mabao 19 kila moja katika mashindano yote wakati Greenwood wamefunga 12 lakini Solskjaer amesema kuwa watatu hao bado wanapaswa kuboresha viwango vyao.

"Unahitaji ushindani kwa maeneo United. Ikiwa unafikiria unayo haki ya kucheza kila mchezo na unafanya vizuri sana kwamba hatutatafuta wachezaji ili kukubadilisha, uko katika nafasi mbaya , "Solskjaer aliwaambia waandishi wa habari.

"Siku zote tunapaswa kuangalia kuboresha, na ikiwa hawafanyi vizuri tunaweza kulazimika kuangalia mahali pengine ili tuwe bora kwa sababu lazima tuwe bora."

Solskjaer amesema alionyesha imani kwa washambuliaji wake wachanga baada ya kumruhusu Romelu Lukaku kujiunga na Inter Milan mnamo Agosti.

"Mwishowe ndivyo unavyofikia kiwango kingine, kiwango tofauti wote watatu (Martial, Rashford na Greenwood) wamekuwa na maendeleo mazuri msimu huu lakini wanaweza kuwa bora zaidi."

Manchester United, wapo nafasi ya sita kwenye msimamo wa Ligi Kuu wakiwa na alama 49, leo watacheza na Brighton & Hove Albion.