14 Jan 2020 / 151 views
Begovic ajiunga AC Milan

Kipa wa Bournemouth Asmir Begovic amejiunga na klabu ya AC Milan kwa mkopo wa msimu mmoja baada ya kufuzu vipimo vya afya.

AC Milan anahitaji golikipa baada ya kumruhusu Pepe Reina ajiunge na Aston Villa kwa mkopo wa msimu wote kwenye klabu hiyo.

Begovic, 32, ameichezea Bournemouth mara 62 baada ya kujiunga nao kutoka Chelsea mnamo 2017, akiwa amecheza pia Stoke na Portsmouth.

Aaron Ramsdale, 21, amekuwa chaguo la kwanza kwa bosi wa Bournemouth Eddie Howe msimu huu, na Mark Travers, 20, aliyechaguliwa wakati haipatikani.

AC Milan itashuka dimbani leo kumenyana na klabu ya Cagliari kwenye michuano ya kombe la Coppa Italia kaika uwanja wa San Siro.