Gurdiola atamani kufundisha klabu ya Italia
Kocha wa Manchester City, Pep Guardiola amesema kuwa yupo tayari kujiunga na ligi ya Italia mkataba wake na Mabingwa hao wa Uingereza utakapomalizika.
Mkataba wa bosi wa City utaisha mwishoni mwa msimu ujao kwani amesaini mkataba wa miaka minne kuifundisha timu hiyo.
Guardiola amewahi kusisitiza kuwa anafurahi maisha kwenye kilabu hiyo na hafikirii kuhusu kuondoka kwenye klabu hiyo.
Gurdiola ilicheza kwa msimu mmoja huko Serie A katika klabu ya Brescia kama mchezaji na haingeruhusu kurudi Italia kama meneja.
"Ilikuwa ni raha kuwa huko kama mchezaji kwani nilikuwa na wakati mzuri na ninaipenda nchi lakini sasa najisikia vizuri kuwa hapa Uingereza’ Alisema Gurdiola.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 48 alivumishwa kujiunga na Juventus msimu wa joto lakini amekanusha kuwa aliwahi kutakiwa na mabingwa hao wa Italia.
City wameshinda mechi moja tu huko Liverpool tangu mwaka 1981 na hiyo ilikuwa nyuma mnamo mwaka 2003.