11 Sep 2019 / 96 views
UEFA kuwashtaki shirikisho la Ufaransa

Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa) siku ya Jumanne ilifungua kesi dhidi ya Shirikisho la Soka la Ufaransa (FFF) baada ya kuchelewa kuanza kwa mechi dhidi ya Albania kwenye mechi ya Euro 2020.

Mechi hiyo ilichelewa kuanza baada ya wachezaji wa timu ya taifa ya Albania kugomea kuanza kucheza mpira mpaka kupigwa kwa wimbo wao wa taifa kutokana na kuchanganya wimbo na kupigwa wimbo wa Andora.

Wasimamizi wa mechi hiyo walicheza wimbo wa Andora kwa kukosea mbele ya mchezo uliofanyika katika uwanja wa Stade de Ufaransa Jumamosi.

Baada ya Waalbania wenye hasira kuandamana, wimbo sahihi ulichezwa na mchezo ukaanza kwa zaidi ya dakika tano na ule muda uliotakiwa kuanza kwa mchezo huo.

Kamati ya Nidhamu ya Uefa, ambayo inachunguza kucheleweshwa yoyote kuanza, imearifu FFF na kesi hiyo itasikilizwa tarehe 17 Oktoba.

Adhabu kawaida ni onyo la kosa la kwanza na faini kwa kosa hilo kutokana na kucheleweshwa kwa mechi hiyo ya kufuzu michuano ya kombe la mataifa ya Ulaya Euro itakayofanyika mwakani barani Ulaya.

Michuano ya mataifa ya Ulaya mwakani (Euro) itafanyika katika miji kumi na mbili katika nchi tofauti barani Ulaya ikiwa ni miaka 60 toka kuanza kuanza kwa michuano hiyo ya mataifa ya Ulaya.